MOURINHO APEWA DILI MAN UNITED VS LIVERPOOL.

Saturday octoba 19 2019 
Na mwandishi  Christer Shechambo

Jose MOURINHO anatarajiwa kuwa mchambuzi wa michezo  kesho jumapili kati ya Manchester United dhidi ya Liverpool.

Uamuzi you umechukuliwa na kituo cha runinga cha sky sports  ambapo baadhi ya mashabiki wa Manchester United  wameshangazwa nakuamin itakuwa ni nafasi ya kocha huyo  kuendelea kuiponda united. 

Mchezo kama you ndio ambao ulisababisha united kumfukuza kazi  mourinho, decemba mwaka jana  baada ya liverpool kushinda bao 3-1.timu hizo zinakutana  huku kukiwa na presha kubwa kwa kocha wa United Ole Gunnar Solskjaer kutokana na matokeo mabaya ya simu huu.

 Inaaminika kuwa historia inaweza kujirudia kwa solskjaer kupoteza kazi kama ilivyokuwa kwa mourinho ikiwa timu yake itapata kipigo likali kutoka kwa wapinzani  wao wa jadi.

Kocha wa liverpool Jurgen Klopp anatarajiwa kuingiza kikosi kikiwa na nguvu kwa kuwa timu yake imekuwa ikifanya vizuri tangu kuanza kwa msimu huu licha ya kuwa mchezo utapigwa kwenye uwanja wa  old Trafford  ambapo ni ugenini kwao.

Washabiki wengi mtandaoni  wametoa maoni ya kushazwa na uamuzi huo wa sky kumpa nafasi mourinho kuchambua mchezo huo huku  wale wapinzani wa United wakifurahia  kwa kuwa na hamu ya kusikia  atakachozungumza.